Sunday, 27 July 2008
KIGOLI AINGIA MTINI
Klabu ya yanga leo iliingia mtini katika mechi ya kutafuta mshindi wa tatu kombe la CECAFA kagame cup hivyo mahasimu wao Simba hivyo basi simba walijinyakulia nafasi hiyo ya tatu kwa bao 3 na pointi 3, lakini bado ni aibu hamna mcheza kwao hata mmoja fainali.
Saturday, 26 July 2008
WAKANADA HOI KWA USA

Katika game hiyo Dwyane Wade, Carmelo Anthony na Michael Redd swalichoma vikapu 20 kila mmoja wao kuwaadhibu Wakanada hapo Las Vegas. mpaka mapumziko walikuwa wakiongoza kwa 61-38 Kobe Bryant aliongeza pointi 15 , Deron Williams 14 na Chris Paul alichoma 11 na assist 8 , wakati wakanad a aliyejitahidi kidoga alikuwa Jermaine Anderson aliyeambulia pointi 18 pointshivyo hadi mwisho wa mchezo usa walishinda 120 - 65 .
Hii ilikuwa ni moja kati ya mechi zao za matayarisho kwa ajili ya olimpiki naona mwaka huu wana kikosi cha ukweli .
MARA NYINGINE TENA
Lewis Hamilton aliwanyuka Heikki Kovalainen, Felipe Massa na Nelson Piquet katika dakika za mwisho na kufanikiwa kujisindia German Grand Prix huko Hockenheim Ujermani 21.07. Huu ni ushindi wake wa pili mfululizo na sasa anaongoza kwa pointi nne mbele ya Massa . Piquet alimaliza akiwa wa pili hii ni podium yake ya kwanza , Massa akiwa wa tatu wakati Kimi Raikkonen alikuwa wa sita
JANGWANI SASAMBU
Kikosi cha vijana wa jangwani
Timu ya Yanga jana iliyojitosa katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Kagame dhidi ya Tusker ya Kenya iliyofanyika Uwanja Mpya, Dar es Salaam jana , ilipigwa kimoko tu bila majibu 1-0. Hivyo sasa Simba na Yanga watakutana katika mchezo mshindi wa tatu ambaye atajinyakulia zaidi ya Sh milioni 12 , katika mchezo huo ambao utakuwa wa utangulizi kabla ya fainali ambayo itaikutanisha URA ya Uganda na Tusker ya Kenya, mshindi wa pili atachukua Sh milioni 23 na ushee na bingwa ataondoka na Sh milioni 34 hivi. Ni aibu hamna timu ya wenyeji fainali nahii inaweza kuzidi kutushusha katika msimamo wa soka duniani. AIBU
MNYAMA ANG'OLEWA MENO
Timu ya Simba alhamisi hii iliyaaga mashindano ya baada ya kuchapwa 1 - 0 , na URA ya Uganda kama haitoshi kuonyesha kuwa mnyama huyo amekuwa wa kibisa sasa wakampa apige penalti ambayo ingewawezesha kurudi katika gemu mchezaji aliyetua siku si nyingi kisa ni mnigeria Izechukwu Emeh naye akamwaga hivyo mnyama nje.
Wednesday, 9 July 2008
HAMILTON KIDEDEA

Lewis Hamilton (MCLAREN) Jumapili hii alijishindia British Grand Prix katika uwanja wa nyumbani Silverstone pamoja na hali ya mvua iliyokuwa ikiendelea na hivyo kuwa juu katika msimamo huo wa formula one katika mashindano hayo alifuatiwa na Nick Heidfeld (BMW )na watatu ni Ruben Barrichello (HONDA) , kwa matokeo hayo anaongoza msimamo akiwa na pointi 48 sawa na
Felipe Massa (Ferrari), Kimi Räikkönen
Felipe Massa (Ferrari), Kimi Räikkönen
Wednesday, 2 July 2008
TIMU BORA DUNIANI
Shirikisho la soka duniani FIFA limetangaza timu bora duniani na katika msimamo huo hispania kwa mara ya kwanza wamesimama katika namba moja. kma msimamo unavyoonyesha hapo chini nafasi nzao na kwenye mabano ni nafasi walizokuwa awali:
1. (4) Hispania, 2. (3) Italia, 3. (5) ujerumani, 4. (2) Brazili, 5. (10) Netherlands, 6. (1) Agentina, 7. (15) Croatia' 8. (6) Ucheki, 9. (11) Ureno, 10. (7) Ufaransa, 11. (24) Urusi, 12. (12) Romania, 13. (13) Cameruni, 14. (20) Uturuki, 15. (9) Uingereza, 16. (17) Skotlandi, 17. (18) Bulgaria, 18. (8) Ugiriki, 19. (14) Mexiko, 20 (16) Ghana, timu iliyoingia katika 20 bora ni Urusi na timu iliyotoka ni Colombia, Africa ya mashariki ni Kenya 92 nafasi 23 juu, Uganda 97 nafasi 2 juu, Tanzania ni115 nafasi 14 chini.
1. (4) Hispania, 2. (3) Italia, 3. (5) ujerumani, 4. (2) Brazili, 5. (10) Netherlands, 6. (1) Agentina, 7. (15) Croatia' 8. (6) Ucheki, 9. (11) Ureno, 10. (7) Ufaransa, 11. (24) Urusi, 12. (12) Romania, 13. (13) Cameruni, 14. (20) Uturuki, 15. (9) Uingereza, 16. (17) Skotlandi, 17. (18) Bulgaria, 18. (8) Ugiriki, 19. (14) Mexiko, 20 (16) Ghana, timu iliyoingia katika 20 bora ni Urusi na timu iliyotoka ni Colombia, Africa ya mashariki ni Kenya 92 nafasi 23 juu, Uganda 97 nafasi 2 juu, Tanzania ni115 nafasi 14 chini.
Tuesday, 1 July 2008
KILA KITU SPAIN

Baada ya Euro 2008 sasa euro 2012 ni Poland Ukraine. Spain ndio kama vile wametoa gundu mabingwa wao vilevile Mfungaji bora ni wao David Villa, Mchezaji bora a mashindano ni Xavi Hernandez, wana wachezaji 9 bora katika timu ya mashindano,
Golikipa: Gianluigi Buffon (Italia), Iker Casillas (Spain), Edwin van der Sar (Uholanzi)
Mabeki: Bosingwa (Ureno), Philipp Lahm (Ujerumani), Carlos Marchena (Spain), Pepe (Ureno), Carles Puyol (Spain), Yuri Zhirkov (Urusi).
Viungo: Hamit Altıntop (Uturuki), Luka Modrić (Croatia), Marcos Senna (Spain), Xavi Hernández (Spain), Konstantin Zyryanov (Urusi), Michael Ballack (Ujerumani), Cesc Fàbregas (Spain), Andrés Iniesta (Spain), Lukas Podolski (Ujerumani), Wesley Sneijder (Uholanzi).
Washambuliaji : Andrei Arshavin (Urusi), Roman Pavlyuchenko (Urusi), Fernando Torres (Spain), David Villa (Spain).

Mfungaji bora David Villa
Wafungaji bora ni
4 -David Villa,
3 - Hakan Yakin, Semih Şentürk, Roman Pavlyuchenko, Lukas Podolski.
2 - Daniel Güiza, Ivan Klasnić, Zlatan Ibrahimović, Robin van Persie, Ruud van Nistelrooy, Nihat Kahveci, Andrei Arshavin, Wesley Sneijder, Arda Turan, Bastian Schweinsteiger,Fernando Torres, Miroslav Klose, Michael Ballack,
1 -Václav Svěrkos, Ivica Vastic, Klaas Jan Huntelaar, Rubén de la Red, Hélder Postiga, Ricardo Quaresma, Arjen Robben, Uğur Boral, Ivica Olić, Raul Meireles, Jan Koller, Dmitri Torbinski.
Magoli ambayo kila timu imejifungia ni :
12-Spain, 10-Uholanzi, Ujerumani, 8 - Uturuki, 7 - Ureno, Urusi, 5 - Croatia, 4 - Ucheki
3 - Sweden,Uswisi na Italia, 1 - Austria, Ufaransa, Ugiriki, Poland na Romania
MBONGO BINGWA WA DUNIA

Hii ilikuwa Jumapili tarehe 29.06.08 ndani ya Diamond jubilee ambapo mbongo japhet Kaseba ailshinda pambano hilo na kutetea ubingwa wa Dunia wa mchezo wa Kick Boxer, picha chini akiwa na mkanda huo wa ubingwa wa dunia unaotambuliwa na Chama cha Kickboxing Ulimwenguni (WKL), mara baada ya kumdunda mpinzani wake, Ricky Agayas kutoka Ufilipino katika raundi ya pili, katika ukumbi wa Diamond, Jubilee, jijini Dar pamoja nae ni baba yake Kaseba Matete kulia pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abass Kandoro.

Sunday, 29 June 2008
SPAIN BINGWA
Thursday, 26 June 2008
FAB AWAPELEKA SPAIN FAINALI

Wachezaji wa hispaniawakiongozwa na fundi au mtaalam kutoka The Gunners Cesc Fabregas kifua wazi wakishangilia ushindi wao wa bao 3- 0 dhidi ya warusi katika mechi ya nusu fainali , hapa watu uhakika wa kuingia fainali yao ya kwanza baada ya miaka 24, toka pale 1984 walipotinga fainali na kupigwa na wenyeji wafaransa bao 2 - 0 wafungaji wakiwa Michael Platini ambaye sasa ni raisi wa UEFA na Bruno Bellone, ambapo pia Platini alikuwa ni mfungaji bora akijiondokea na magoli 9 ambayo ni recod mpaka leo haijavunjwa , kati ya hayo 9 alikuwa na hat - tricks mbili dhidi ya Yugoslavia na Ubelgiji katika game hizo mbili alifunga magoli kwa style kwani kila game alihakikisha ana goli moja la kichwa, guu shoto na guu la kulia mtoto mtoto huyu aikuwa mbaya . Basi vijana wa Spain ndio vile tena mpaka jumapili dhidi ya wajerumani, magoli yao yalifungwa na Xavi Hernandez,Daniel Guiza na David Silva fabregas akitengeneza mawili pamoja na kuwa alikuwa akicheza nje ya nafasi yake ya kiungo, maana aliingia kama striker kuziba pengo la David Villa anayeongoza kwa magoli.
Wednesday, 25 June 2008
ujerumani fainali
Monday, 23 June 2008
WATU WAMEVUNJA MWIKO

Sunday, 22 June 2008
PAUL INCE

Paul Ince 40 amesaini mkataba wa miaka mitatu kuwa kocha wa Blackburn Rovers kumrithi Mark Hughes (wote hawa ni watoto wa Sir Alex Ferguson). Kijana huyo wa Ilford atakuwa ni kocha Muingereza mweusi wa kwanza ndani ya Premiership, pia aliwahi kuwa muingereza mweusi wa kwanza kukaptain Uingereza ameitosa timu ya MK Dons ambayo msimu uliopita aliisaidia kupanda daraja na pia kushinda Johnstone's Paint Trophy. Ince aliwahi kuzichezea timu maarufu kama Manchester United, Liverpool na Inter Milan kabla ajajimix Middlesbrough , Wolverhampton Wanderers ambayo ilifanikiwa kupanda premier league kwa mchango wake mkubwa, Swindon Town alikuwa kocha mchezaji alafu akaenda Macclesfield Town kama kocha mchezaji ambapo aliwasaidia kutokushuka daraja , kabla ya kuhamia Milton Keynes Dons ambapo aliisaidia timu hiyo kupanda Coca-Cola League 1 mwaka huu.
MOTO GP


Wakati huohuo Mika Kallio nae alijihakikishia kuendelea kuongoza msimamo wa 250cc World Championship aliposhinda kwa mbinde British MotoGP 250cc, hapo hapo Donington Park, ushindi huo ulikuja bila kutegemewaa kwani alianza mashindano hayo akiwa wa 14 akajitahidi kuwapunguza mmoko mmoko hadi robo ya mwisho aliwabakiza 2 mbele yake Alvaro Bautista na Marco Simoncelli ila zikiwa zimesalia lap 2 kama zali jamaa walijaa mmoja kushoto mwingine kulia mtu mzima akajipenyeza kati kama zali ndio vile tena.
FORMULA ONE

Filipe Massa ameshinda French Grand Prix huko Magny-Cours akifuatiwa na Kimi Raikkonen kuhakikisha timu yao ya ferari inajishindia namba moja na mbili, ambapo Jarno Trulli wa Toyota alijishindia nafasi ya tatu podium ya kwanza kwake msimu huu na ya kwanza kwa toyota tangu 2005, wakati ambapo Lewis Hamilton aliyeanza mashindano hayo katika nafasi ya 10 kama penalti kwa kumgonga kimi kizembe katika Canada GP alimaliza akiwa wa wa 11.
Khan bado bingwa
MOTO GP 125cc

Mutoto wa kiingereza Scott Redding leo amekuwa muingereza wa kwanza tangu 1986 kushinda mashindano ya pikipiki yanayoitwa Moto Gp 125cc katika uwanja wake wa nyumbani, akiwa na nashine yake ya Honda 125cc, alishinda kwa sekunde 5.3 baada yakuwa wa pili kwa muda mrefu wa mashindano hayo. Kijana huyo pia ameweka record kuwa mshindi akiwa na umri mdogo wa miaka 15 na siku 170.
Subscribe to:
Posts (Atom)
karibuni wote ndani ya blog hii kwa michezo mbalimbali toka kila kona ya dunia